Translate

Saturday, November 18, 2017

Riwaya: SIKU TATU KABLA
Mtunzi: PIANO MAYA
CONTACT:0687913339
WhatsApp:0656292416
Dar es salaam

                           SEHEMU YA KWANZA(01)



hahhahaa we jamaa unanichekesha sana, baba yako hana hata baiskeli alafu wewe unawaza kumiliki gari, acha fikra potofu na ndoto za mchana kweupe!
ilisikika sauti hiyo ya kijana mmoja aliyekuwa ameongozana na KANGAMBULA,walikuwa marafiki walioshibana,, walisaidiana kwa kila jambo, Kangambula akasema,"nitaendelea kusoma kwa bidii ili niweze kuisaidia familia yangu na kuwasomesha kuwasomesha wadogo zangu..

wakati huo huo upande mwingine, nyumbani kwao kangambula ,,alionekana mwanamke mmoja akiwa anatoa furushi la nguo na kuliweka nje kando ya nyumba,, kisha akazipiga hatua kurudi ndani ya nyumba,, jina lake anaitwa Mbaliwa, ni mama mzazi wa Kangambula. akapitiliza moja kwa moja mpaka chumbani akaketi juu ya kitanda huku akimtazama mumewake kwa macho ya huruma, huku akisema , utapona mume wangu, naimani zile dawa alizokupa daktari zitakusaidia kurudisha afya yako kuwa njema kam awali... mimi pia nakuombea kwa Mungu akuponye upone haraka. mumewe akamtazama kisha akasema,"asante mke wangu, kwani Kangambula bado hajatoka shuleni?
mkewe akatabasamu kisha akasema, unampenda sana mwanao, hii ndio mida yake ya kutoka shule, atakuja muda si mrefu, kabla hajamaliza sentensi, ikasikika sauti ya Kangambula ikimuita mama yake,,
bila kuchelewa Mbaliwa akatoka chumbani akija upande wa sebuleni kumsikiliza mwanae, Kangambula akauliza hali ya baba yake huku uso wake ukionyesha shauku ya kutaka kumuona muda huohuo. Mbaliwa akasema," si njema sana pia alikuwa anakuulizia. Kangambula akazipiga hatua kuingia chumbani kumsalimia baba yake.

   ***************BAADA YA MWEZI MMOJA KUPITA***********

Kangambula akasimamishwa masomo, ni baada ya kushindwa kulipa ada ya muhula uliobaki,, pia mwalimu akasisitiza hatofanya mtihani endapo asipolipia kiasi cha pesa kilichobaki! jambo hilo lilimfanya Kangambula kuwa mnyonge na huzuni ikatawala juu yake, mbaya zaidi, zimebaki siku tatu tu, afanye mtihani wa kuhitimu kidato cha nne.aqkaipokea barua kutoka mikononi mwa mwalimu mkuu,, huku machozi yakimtoka, akajaribu kubembeleza huku akitoa sababu za msingi zilizosababisha ashindwe kulipia kiasi cha pesa iliyobaki kwa ajili ya ada,, lakini mwalimu mkuu hakutaka kusmsikiliza akamfukuza,,"toka ofisini kwangu, Kangambula akatoka akalitazama darasa alilokuwa analitumia kwenye vipindi vya masomo, akashindwa kuvumilia machozi yakamtoka, akalia kwa uchungu wa hali ya juu, rafiki yake kipenzi akamuona Kanagambula akilia, akaamua kumfuata na kumfariiji. lakini haikusaidia faraja hiyo haikuweza kutibu jeraha ndani ya moyo wa Kangambula,, hakujibu kitu,"aliishia kumtazama rafiki yake kisha akaamua kuondoka na kurudi nyumbani.

Kangambula alitembea,lakini alikuwa mbali kifikra, akaamua kupiata njia ya mkato ilimradi awahi kufika nyumbani. kwa mbali akaonekana kijana mmojqa anakimbia kwa kasi ya ajabu huku uso wake ukionyesha wasiwasi maradufu! naye pia alikuwa kavalia suruali yenye rangi kama sale ya shule aliyoivaa Kangambula,, wakati kijana huyo anakimbia akadondosha akatupa begi alilokuwa amelishikilia,, kuku akiendelea kutimua mbio na kutokomea kusikojulikana!
Kangambula akastaajabu sana,, hakujali akaendelea kuzipiga hatua kuelekea nyumbani. akafika karibu na lile eneo ambalo yule kijana alitupa lile begi.
akajisemea moyoni,,"bila shaka huyu ni mwanafunzi katika shule ninayosoma mimi. inamaana kapatwa na ugonjwa wa akili? mbona katupa begi lake? ...Kangambula aliwaza hivyo kwa sababu yule kijana alikuwa kavaa suruali yenye rangi kama aliyovaa yeye! hivyo akaamini ni mwanafunzi... lakini hakujali akaendelea kuzzipiga hatua.. baada ya hatua kadhaa jua lilikuwa kali akaamua kuvua shati la shule na kuliweka ndani ya begi akabaki na t-shirt nyepesi. ghafla wazo likamjia,, akaamua kurudi nyuma kulifuata lile begi alifungue atazame jina la mwanafunzi huyo pamoja na kidato.
alipolikaribia begi hilo akasita kulichukua,, akasimama kwa sekunde kadhaa, huku akilitazama,, akalisogelea na kulichukua akafungua zipu ya begi hilo dogo! akashtuka! macho yakamtoka,, akaangaza macho yake huku na kule huku mikono yake ikitetemeka,, jasho jembamba likaanza kumtoka,,, akaliachia begi hilo kisha akachuchumaa,,, uso wake ukaonyesha kuwa na wasiwasi kupita kiasi. pia bado macho yake yaliendelea kutazama huku na kule! hakuona mtu yeyeote kuwepo eneo hilo. akanyanyuka na kuliacha begi hilo. akatimua mbio kukifuata kichaka kilichokuwa kando akatoa begi lake lenye madaftari na kulificha ndani ya kichaka hicho.. kisha akarudi pale lilipokuwepo lile begi lililotupwa na yule kijana!
akialifungua kwa maranyingine tena.. akameza mafundo kadhaa ya mate. kisha akajisemea moyoni,,"hizi ni pesa kweli au naota ndoto za mchanamchana kweupe?
akazishika pesa hizo ,,akagundua ni pesa kweli..noti za shilingi elfu kumi kumi..akalifunga begi hilo akalichukua na kuliweka mgongoni! akajisemea moyon,," sasahivi naenda kulipa ada yote iliyobaki.. alafu naenda nyumbani kumchukua baba yanguu nimpeleke mjini akatibiwe.. baada ya kuwaza hivyo,, akatabasamu kisha akatimiua mbio kurudi shuleni.. kulipa kiasi chote cha ada iliyobaki.

baada ya nusu saa kupi akaonekana akizipiga hatua za haraka haraka kuelekea katika ile njia alipolificha begi lake la shule. akiwa njiani akastaajabu kuona kundi la watu wakiwa wameshikilia marungu na mapanga miongoni mwa watu hao alionekana mwanamke akili kwa uchungu wa hali yajuu,, Kangambula akajisemea oyoni,,"bila shaka huyo mwanamke katenda kosa hivyo wanamuadhibu,, ghafla ikasikika sauti ya yule mwanamke ikisema kwa msisitizo mwizi mwenyewe yule pale na begi langu analo.. sauti hiyo ilimstua Kangambula baada ya kusikia kali ya mwanamke huyo ikihusisha begi..wakati anatahamaki ghafla akaona lile kundi la watu likija upande wake huku wakipiga kelele MWIZIII MWIZII MWIZII! kangambula akaamua kutimua mbio ghafla akajikwaa na kudondoka chini.

ITAENDELEA............


Ungana nami PIANO MAYA(MAYA wa HADITHI) katika sehemu ya 2

No comments:

Post a Comment