Riwaya: SIKU TATU KABLA
Mtunzi: PIANO MAYA
CONTACT:0687913339
WhatsApp:0656292416
Dar es salaam
Mtunzi: PIANO MAYA
CONTACT:0687913339
WhatsApp:0656292416
Dar es salaam
SEHEMU YA PILI(02)
Akajigonga upande wa kichwani katika jiwe lililokuwa limezama chini ya ardhi, na kuchomoza kiasi upande wa juu ya aridhi, na kupoteza fahamu papo hapo, baada ya sekunde kadhaa kupita, wale watu waliokuwa wameshikilia marungu,mawe pamoja na mapanga wakawa wamefika eneo hilo,, bila kuchelewa yule dada akavuta begi lake kutoka mikononi mwa Kangambula , ,punde si punde wale watu wakataka kumshambulia Kangambula,, ghafla ikasika saauti ya yule dada aliyeibiwa begi ikisema,,"muacheni sio huyu,, hata hafanani na yule kijana aliyeniibia begi langu, aliongea maneno hayo huku akijiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu,, mmoja kati waliokuwemo miongoni mwa kundi hilo akamtazama kwa makini Kangambula akagundua ni kweli sio yeye, akageuza shingo yake na kumtazama yule dada aliyeibiwa begi...kisha akasema,"kwa sababu umeshapata begi lako, hakuna shida, baada ya kauli hiyo watu wakatawanyika kila mmoja akapita njia yake na ukimya ukatawala eneo hilo.
baada ya masaa mengi kupita, Kangambula alionekana bado akiwa kalala pale chini,, punde si punde akashtuka na fahamu zikarejea,, akahisi maumivu makali upande wa kichwani,, akanyanyuka taratibu kwa kujikongoja!akaonekana kushangaa eneo hilo,, akajiuliza hapa ni wapi?
kumbe alivyodondoka chini na kujingonga katika lile jiwe ubongo wake ulitikisika na kumbukumbu zake zikapotea,, kwa sasa hakumbuki jambo hata moja.
kumbe alivyodondoka chini na kujingonga katika lile jiwe ubongo wake ulitikisika na kumbukumbu zake zikapotea,, kwa sasa hakumbuki jambo hata moja.
upande mwingine ,kule nyumbani kwao Kangambula,, alionekana Mbaliwa,,mama mzazi wa Kangambula akiwa na wasiwasi juu ya mwanae,akajisemea moyoni,,"mbona leo kachelewa kurudi nyumbani! yapataa saa kumi na mbili za jioni sasa,, mwanangu kapatwa na nini?
alijisemea maneno hayo akiwa kaketi nje ya nyumba, ghafla ikasikika sauti ya mumewe akikohoa mfululizo,huku akimuita mkewe! sauti hiyo ilitokea chumbani,
Mbaliwa akapata wasiwasi akanyanyuka na kutimua mbio kuelekea ndani ya nyumba akapitiliza moja kwa moja mpaka chumbani...akashtuka kumuona mumewe anajinyoosha kwa nguvu zake zote,,punde si punde akashusha pumzi na kutulia tuli. Mbaliwa akasogea kitandani huku akimuita mumewe,, aliita mara kadhaa huku akimtikisa,, lakini mumewe hakuitika hata hakuamka. ndipo akagundua mumewe tayari kakata roho,, akaangua kilio kwa sauti kali.
alijisemea maneno hayo akiwa kaketi nje ya nyumba, ghafla ikasikika sauti ya mumewe akikohoa mfululizo,huku akimuita mkewe! sauti hiyo ilitokea chumbani,
Mbaliwa akapata wasiwasi akanyanyuka na kutimua mbio kuelekea ndani ya nyumba akapitiliza moja kwa moja mpaka chumbani...akashtuka kumuona mumewe anajinyoosha kwa nguvu zake zote,,punde si punde akashusha pumzi na kutulia tuli. Mbaliwa akasogea kitandani huku akimuita mumewe,, aliita mara kadhaa huku akimtikisa,, lakini mumewe hakuitika hata hakuamka. ndipo akagundua mumewe tayari kakata roho,, akaangua kilio kwa sauti kali.
Asubuhi palipokucha taratibu za mazishi zikafanyika lakini mpaka muda huu Kangambula hakuwepo nyumbani, pia hajui kama baba yake amefariki! jambo hilo lilizidi kumchanganya sana Mbaliwa,, lakini hakukata tamaa ya kumsubiri mwanae aje nyumbani wajumuike kumzika baba yake!
masaa yalizidi kusonga hatimae muda wa kuzika ukafika lakini hakuna dalili yoyote ya Kangambula kurudi nyumbani,,ikalazimika watu waende kumtafuta Kangambula aje kumzika baba yake. lakini hawakufanikiwa kumpata ... kadri masaa yalivyozidi kusonga ndivyo, maiti ya baba Kangambula ilizidi kuharibika na kutoa harufu kali.. ikalazimika azikwe muda huohuo,,na mazishi yakafanyika.
masaa yalizidi kusonga hatimae muda wa kuzika ukafika lakini hakuna dalili yoyote ya Kangambula kurudi nyumbani,,ikalazimika watu waende kumtafuta Kangambula aje kumzika baba yake. lakini hawakufanikiwa kumpata ... kadri masaa yalivyozidi kusonga ndivyo, maiti ya baba Kangambula ilizidi kuharibika na kutoa harufu kali.. ikalazimika azikwe muda huohuo,,na mazishi yakafanyika.
baada ya siku kadhaa kupita ,,Mbaliwa alikuwa katika majonzi mazito ya kumpoteza mume wake kipenzi,, mbaya zaidi haijulikani ni wapi alipo mwanae!
siku zilizidi kusonga na miezi ikakatika,,hali ya maisha ya familia ya Mbaliwa ikaanza kubadilika! maisha yakawa magumu kwa upande wake,,wakati mwingine walikosa pesa ya kununulia chakula,siku ya leo,Mbaliwa aliwatazama watoto wake wawili aliobakinao nyumbani,,akajikuta analia kwa sababu bado wadogo hawawezi kujitegemea!
************************************
baada ya miaka kumi kupita,, akaoneka kijana mmoja akiwa amebeba mifuko miwili mikubwa,, akazipiga hatua kuufuata mkokoteni wake na kuweka mifuko hiyo iliyojaa takataka,, kisha akaondoka zake..mtu huyo si mwingine ni Kangambula mwenyewe. kumbe miaka hiyo yote alikuwa mjini akifanya kazi ya ubebaji taka kwa malipo.
siku ya leo alifanya kazi ya kubeba taka mpaka majira ya saa kumi za jioni,,katika pitapita zake akagonga hodi katika geti la nyumba iliyokuwa imejitenga... nyumba hiyo ilionekanakumilikiwa na tajiri kutokana na uzuri wa jengo la nyumba hiyo! Kangambula aligonga geti hilo kwa mara kadhaa lakini hakuna alikuja kufungua geti hilo,, akaamua kuchukua mfuko uliokuwa na takataka kando ya geti hilo,,kisha akajisemea moyoni,,"kesho nitakuja kuchukua pesa yangu ya kubeba takataka hizi..akabeba mfuko huo na kuondoka zake..kabla hajafika mbali, akastaajabu kuona magari yamebeba maaskari katika njia hiyo anayopita yeye, akatoka barabarani na kusimama kando ya barabara...akasimama huku akitazama magari hayo,, akaona yamesimama nje ya lile jumba la kifahari..punde si punde maaskari hao wakavamia na kuingia ndani ya jumba hilo huku maaskari wengine wakiwa wamebaki upande wa nje wameshikilia bunduki zao.
Kangambula akaamua kuondoka zake.. akasukuma mkokoteni wake kwa pupa,,ghafla ule mfuko ukadondoka na takataka zote zikamwagika chini Kangambula akashtuka kuona kisu kikiwa na damu pamoja na bastola,,macho yakamtoka,,wakati anatahamaki ikasikika sauti ikisema,"............
siku ya leo alifanya kazi ya kubeba taka mpaka majira ya saa kumi za jioni,,katika pitapita zake akagonga hodi katika geti la nyumba iliyokuwa imejitenga... nyumba hiyo ilionekanakumilikiwa na tajiri kutokana na uzuri wa jengo la nyumba hiyo! Kangambula aligonga geti hilo kwa mara kadhaa lakini hakuna alikuja kufungua geti hilo,, akaamua kuchukua mfuko uliokuwa na takataka kando ya geti hilo,,kisha akajisemea moyoni,,"kesho nitakuja kuchukua pesa yangu ya kubeba takataka hizi..akabeba mfuko huo na kuondoka zake..kabla hajafika mbali, akastaajabu kuona magari yamebeba maaskari katika njia hiyo anayopita yeye, akatoka barabarani na kusimama kando ya barabara...akasimama huku akitazama magari hayo,, akaona yamesimama nje ya lile jumba la kifahari..punde si punde maaskari hao wakavamia na kuingia ndani ya jumba hilo huku maaskari wengine wakiwa wamebaki upande wa nje wameshikilia bunduki zao.
Kangambula akaamua kuondoka zake.. akasukuma mkokoteni wake kwa pupa,,ghafla ule mfuko ukadondoka na takataka zote zikamwagika chini Kangambula akashtuka kuona kisu kikiwa na damu pamoja na bastola,,macho yakamtoka,,wakati anatahamaki ikasikika sauti ikisema,"............
ITAENDELEA......
Ungana nami PIANO MAYA katika sehemu ya 3



